SETTA Iftar Gala - 2026.
SETTA Iftar Gala - 2026. Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Dkt. Bëkir GEZËR, alihimiza ushirikiano uliopo kati ya Uturuki na Tanzania, pamoja na kugusia umuhimu wa mahusiano baina ya nchi mbili (Uturuki na Tanzania) ambayo yanaendelea kukua katika nyanja mbalimbali za kimkakati ikiwemo Elimu, Biashara, Miundombinu na Afya. Aidha, Mh. Balozi alieleza kuwa hafla hiyo inalenga kuimarisha mtandao wa mahusiano kati ya wahitimu wa Uturuki, taasisi pamoja na wadau mbalimbali wa Kituruki kwa ajili ya kuendeleza ushirikiano katika nyanja tofauti za maendeleo baina ya Uturuki na Tanzania. Pia, Mh. Balozi amekuwa mfano halisi wa ushirikiano wa Uturuki na Tanzania katika nyanja za Kijamii kwa kuendana na utamaduni wa kuzungumza lugha ya Kiswahili. Cc. @tnzbe.bekirgezer @tc_darusselambe @alumniturkiye



