Mkutano na Balozi wa Uturuki
Mkutano huu utakuwa na ugeni maalumu kutoka kwa Alumni ambao ni Wadau wa Sekta ya Afya katika kushirikishana Fursa na Elimu katika Sekta ya Afya. Aidha, mkutano huu utaambatana na zoezi la Uchangiaji wa Damu kwa kushirikiana na wadau wa Taasisi ya Tujuane Hub na Mpango wa Taifa wa Damu Salama – Tanzania. Pia, mkutano huu utatoa majibu na njia ya kupata suluhisho la changamoto mbalimbali wanazopata Türkiye Alumni kupitia ushirikiano baina ya Tanzania na Uturuki.



