Tanzania Türkiye Alumni Iftar Gala Highlights
SETTA Iftar Gala - 2026 Highlights. Katika kuadhimisha mwezi Mtukufu wa Ramadhan, Taasisi ya SETTA ikishirikiana na Ubalozi wa Uturuki Tanzania, iliandaa hafla ya Iftar Gala kwa Wahitimu wa Uturuki nchini Tanzania. Hafla hiyo ilihudhuriwa na Mgeni Rasmi Mh. Balozi Mhandisi Zena Ahmed Said (Katibu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Saudi Arabia) pamoja na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Mh. Dkt. Bekir GEZËR. Aidha, Katika hafla hiyo Mh. Balozi Mhandisi Zena Ahmed Said, alisisitiza juu ya Ufadhili wa Misaada ya Kibinadamu kupitia taasisi ya SETTA ilikuweza kuwafikia walengwa husika na katika jamii kubwa ya watu wenye uhitaji. Pia, Misaada hiyo iweze kugusa maisha ya wahusika katika kuwakwamua kutoka katika umasikini na kuchochea maendeleo ya jamii ya Kitanzania. Balozi wa Uturuki nchini Tanzania (Mh. Dkt. Bekir GEZËR) ameahidi kuendeleza ushirikiano na Wahitimu wa Uturuki katika kuimarisha mahusiano baina ya Uturuki na Tanzania. Cc. @zenasaidzas @tnzbe.bekirgezer @tc_darusselambe @alumniturkiye @yurtdisiturkler



